Please send your suggestions to uswahili@aol.com

Thursday, January 28, 2010

Shosti! naomba moto!!

When unaona uvivu kununua boksi ya kibiriti ya kuwashia moto kwenye jiko la mkaa, alafu kila siku unamgongea hodi jirani yako asubuhi eti "shosti! naomba moto?" Wengine eti naomba chumvi, nyanya, vitunguu, dah, kama vile amefika supa maketi!!!

8 comments:

  1. Na pia ndio hao hao ambao kila siku wanaomba ndala kwa jirani. Ukiwanyima wanasema "oh! vitu vidogo tu hivyo unatubania". Jamani, kama unahitaji ndala kwa nini usinune zako? Na kama ni "vitu vidogo", mbona huna?

    ReplyDelete
  2. Inaonyesha mwenye blogu hujaishi uswahilini na hujui mazingira wala maadili ya huko uswahilini. Suala la kuomba moto sio kuwa ndani huna kibiriti, ni socialization tu, mtu anaona rahisi kuchukua moto, tunaita kupaa moto kwa jirani, na huwezi kwenda kupaa moto nyumba yoyote ile lazima utaenda kwa watu ambao mko karibu, mna kaushoga fulani, na huingii kupuru eti naomba moto.

    Hebu jiulize maisha ya uswahilini hakuna umeme, kama mtu hana kibiriti anawashaje taa yake ya chemli au kibatari usiku? Na usiku huruhusiwi kuomba moto kwa jirani, hata chumvi haiombwi kwa jirani.

    Ninavyoona bora utafute mtu anayeishi uswahilini akusaidie kujua kwanza kwanini vitu vinatendeka kihivyo uswahilini au kijijini, maana hata vijijini watu wanapaa moto kwa majirani zao. Kisha ndio uandike, hata msomi wa anthropology aliyetoka Ulaya ambae sio muafrika anaweza kuja na good reasoning kuliko hiyo yako.

    Nilipoona blog ya uswahili, nikajua angalau na sie waswahili tumepata mahala pa kujidai kuelezea kwa nini vitu vinatendeka jinsi vinavyotendeka uswahilini, kumbe sivyo kabisa, naona lengo ni muendelezo wa dharau na kashfa kwa waswahili. Ngoja nifungue blogu ya kweli ya waswahili uone jinsi watu watakavyojaa kujifunza humo mambo mengi yanayohusu maisha ya kiswahili/kiafrika na si hayo mnayoiga ya tamaduni za wageni ya kiselfish ya kila mtu kivyake vyake mwishoe watu wanaishia kuwa na depression kwa sababu hawapati mahala pa kurelease stress zao hawana social networks kama hizo za waswahili


    Mswahili

    ReplyDelete
  3. Mdau Mswahili, nakubaliana nawewe kabisa katika swala la kuomba moto uswahilini, lakini inategemea, kama mtu anaishi kijijini bila umeme hiyo ni sawa kabisa. Hapa namaanisha wale wa mjini ambayo wanauwezo kabisa wakununua hizo vitu vidogo-vidogo.

    You are totally welcome to start your own blog, if you want to explain and defend why they do that. I will be happy to share the link on this blog. My intention is just to share those experiences as an inside joke for those who understand they will just laugh it out and take it simple.

    Remember most of the posts here are contributed by members of the group on facebook. This is just a collection of what they had to say.

    ReplyDelete
  4. hiyo socialism ni ya kipuuzi na inalemaza........coz watakuwa hawajifunzi kununua vi2 vyao.....kama ukiomuomba mzungu samaki sikuya kwanza atakupa lakini ya tatu anakupa ndoano bila hivyo utakufa maskini......m2 akiomba moto mwambie akupe mkaa wa ku replace muende sawa ndo atajifunza......

    daver

    ReplyDelete
  5. Hi most of the post here seem to be old than a month, probably there are nu post which i can not see them here but to add on the above "mstaafu rais mkapa alisema recently... watanzania ni wavivu wa kufikiri ..what to do.. that`s why we are remaining the same for decades and put too much complains on the leaders`s shoulders.!!!! hivyo nakubaliana nawe daver kua teach them to fish not giving them fish.

    ReplyDelete
  6. Ni mshangao ulonipata, sijui ni ulimbukeni wangu but any body tell me if ni ulimbukeni! nimesikia chama tawala kinafanya fundrising ili kupata pesa za kampeni..! na lengo ni kupata bilioni arobaini!!! 40 Bilions!! only to get him sit in the white house again!!!, kwa ushamba wangu nikafanya mahesabu ya haraka haraka maana mi ni mchaga bwana... nikakuta watanzania kwa mahesabu ya haraka haraka tupo milioni 40. hii inajumlisha watoto na baba na mama zao.. sasa nikafikiri tena kwa haraka haraka kati ya bilioni 40 tukijaribu kumpatia kila mtanzania milioni 2 x 40 ni milioni 80. from 40 bilion?, nikapata ni pesa kidogo sana zitapungua then nikasema kwa mahesabu yangu ya kichaga, je hii haitakua kampeni bora kupita zote kwa kuwaondole watanzania umasikini???? na ninaamini wananji wangekichagua kiyama tawala bila kufanya kampeni!!!. well, nimeongea sana hebu nisaidieni.

    ReplyDelete
  7. Wow, that's what I was looking for, what a stuff! existing here at this web site, thanks admin of this web page.

    Feel free to surf to my blog post bathroom remodeling

    ReplyDelete
  8. ww mwenye blog umekakaa uswahilini sana if not, umejuaje kama uswahilini kuna kuombana moto! After all kuishi uswahilini is just a part of the jouney to destinations of life changamoto za uswahilini isiwe ni chanzo cha kubeza na kudharau makazi ya uswahilini hasa wanawake! Ila muhimu ni kujifunza na kutambua na kuthamini uwezo na mchango wa watu wa uswahilini ktk jamii pia kuweka bayana madhara na mazingira hatarishi in uswazi. Mswazhili me like ur comments!

    ReplyDelete